Muigizaji wa filamu Shamsa Ford
amefunguka na kusema kwamba tangu aachane na Ex boyfriend wake Dickson
Matoke aliwahi kuwatishia kuwauwa yeye na mwanae zaidi ya mara 10.
Akizungumza na millardayo.com alisema…’Ni
kweli wakati nilipokuwa katika mahusiano naye alikuwa ni mtu ambaye
anapenda sana kuniambia neno nitakuuwa mimi na mwanangu ndio maana
nilikuwa naogopa sana kwasababu nilihisi kuwa anaweza kufanya lolote
kunikomoa na nilienda hadi polisi kuchukua RB yake ili kama lolote
litakalotokea basi yeye atakuwa amehusika, yaani yule alikuwa ananiambia
kabia yuko serious mbaya kuwa ataniuwa mimi na mtoto wangu lisha kwangu
alikuwa anawaambia hata marafiki zangu ni mashahidi na mbaya zaidi
alikuwa anasema hayo maneno na mbaya zaidi alikuwa anawaambia hata ndugu
zake.
Shamsa akiwa na ex-boyfriend wake
Hayo maneno alikuwa anayaongea wakati
bado niko naye kwenye uhusiano lakini ndio hivyo malumbano malumbano na
mimi nilikuwa nimeshachoka na hizo tabia zake lakini baada ya kuachana
naye ni vitisho labda anataka kumuona mtoto anatumia vitisho mara sasa
ninapomnyima mtoto basi anatumia vitisho basi mimi nikikumbuka lile neon
lake la kusema ataniuwa basi moyoni sina amani….’alisema
No comments:
Post a Comment