Tuesday, November 12, 2013

TONYA BUSINESS AAIBIKA,SOMA HII

Mwanamuziki nyota wa muziki wa kizazi kipya usiku wa kuamkia Jumatatu alionja joto ya jiwe baada ya kutekwa na kusurubiwa kisha kunyang'anywa kila kitu pamoja na gari yake.



Mwanamuziki huyo akiwa kwenye viunga vya Club ya usiku ya Kibo iliyopo Tegeta Jijini Dar pamoja masista du wakila bata ghafra kundi la watu watano lilimvamia na kumkamta msobe msobe hadi nje ya ukumbi pamoja na kumrukisha kichurachura huku wakina dada waliokuwa wamendamana nao wakilia kwa uchungu kwa kumuonea huruma.

Habari zaidi toka kwa chanzo chetu kilichoshuhudia timbwiri hilo kilisema kuwa chanzo cha tukio hilo ni kudaiwa kwa Matonya na mtoto wa mjini aliyefahamika kwa jina la Evance" Huyu Evance ni mtoto wa mjini na huwa anawakopesha pesa wanamuziki mbalimbali pamoja na wasanii wa bongo movie hivyo miezi ya hivi karibuni alimkopesha shilingi laki nne msanii huyo kwa madai kuwa hakuwa na pesa ya kula bata wikiendi ambapo baada ya kumkopesha msanii alianza kuzungusha kurudisha hali iliyomfanya Evance kuchukua hatua za kumfanyia unyambilisi huo" Kilisema chanzo chetu


WEMA ASITEGEMEE KUOLEWA NA MIMI-by DIAMOND



 
 
 
 
Stori: Musa Mateja    

RAIS wa Wasafi Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’, juzikati alifunguka kuwa kwenye maisha yake ya ndoa atakayoingia siku chache zijazo, aliyekuwa mchumba wake wakamwagana na kurejeana hivi karibuni, Wema Sepetu asitegemee kuolewa naye.
Diamond ambaye ni staa wa Bongo Fleva aliyasema hayo mbele ya paparazi wetu Novemba 7, mwaka huu jijini Dar kufuatia kuulizwa anamchagua nani wa kumuoa kati ya Wema Sepetu na mchumba wake wa sasa, Penniel Mungilwa ‘Penny’.
Swali kwa Diamond liliibuka baada ya kuzagaa kwa tetesi kwenye mitandao ya kijamii kwamba yu mbioni kumvisha pete ya uchumba mmoja wa mademu zake.
Swali hilo lilimfanya Diamond afunguke kwa kusema kwamba anachokijua yeye na ambacho kipo kwenye mikakati yake, mke wake mtarajiwa ni Penny.
“Najua wengi wanahisi mimi ninaweza kuoa mwanamke zaidi ya mmoja kutokana na dini yangu kuruhusu lakini jambo hilo mimi silifikirii hata kidogo kwa kuwa kwenye maisha yangu nilishapanga nitaoa mke mmoja tu,” alisema Diamond.
Akaendelea: “Watu wanasema mengi juu yangu na Wema, wengi wao hawajui nafsi yangu inataka mwanamke yupi, ninachoweza kusema na watu wakasikia na kunielewa basi wajue kwamba Penny ndiye mke wangu, Wema asitegemee kuolewa na mimi.”
Diamond alikwenda mbele zaidi kwa kumwanika Penny kwamba ana sifa ya kuwa mke kwani ni mvumilivu sana na anaonesha upendo wa dhati kwake.
“Kwa maana hii basi hakuna mwanamke mwenye jina  kubwa wala sura nzuri zaidi ya Penny ninayeweza kumwita mke wangu. Najua kila mtu ana namna yake ya kuchagua ampendaye, ndiyo maana utaona watu wanasema hili mara lile, lakini hawajui nafsi yangu inataka mwanamke wa aina gani,” alisema Diamond na kuongeza:
Kama kuna demu anayejipa matumaini hayo basi asitegemee hata siku moja kwa sababu kuoa kwangu kutazingatia mke mwema na si bora mke, Penny pekee ndiye mwenye sifa za kuwa mke wangu,” alisema Diamond.
Juzi Ijumaa Wikienda lilimpigia simu Penny ili kutaka kupata maoni yake kuhusu tamko la Diamond, lakini muda mrefu simu hiyo ilikuwa ikiita bila kupokelewa.
Baada ya kumkosa Penny, Ijumaa Wikienda lilimtwangia simu Wema, naye kama Penny, simu yake iliita mara kadhaa lakini haikupokelewa

 

HUYU NDIO KAMA WA WAASI WA M-23,SOMA WASIFU WAKE


 

Kanali Makenga alizoea kutembea na bakora, ishara kuwa alikuwa mfugaji na pia kamanda wa kijeshi aliyetaka majeshi yake kuwa na nidhamu na kumtii. 


Mrefu na mwembamba , Makenga alikulia katika maeneo ya milimani mkoani Kivu Kusini ndani ya Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, na alisifika sana kwa kuwa mlenga shabaha na mtu mwenye maarifa na mwenye ujuzi wa kupanga mambo ya kijeshi.

 

Alipata ujuzi wake wa kijeshi nchini Rwanda, ambako alikuwa mmoja wa wapiganaji wa Rais Paul Kagame kabla ya kuchukua mamlaka mjini Kigali.

Baadaye alirejea DR Congo na kuwa mtu mashuhuri katika harakati za kudai haki za wenyeji wa Tutsi wa Congo ambao pia ni wachache.

Maisha ya Kanali Makenga kama mwanajeshi yalifana sana wakati wanajeshi wa M23 walipoteka mji wa Goma , Mashariki mwa DR Congo.

Pia alimshinda hasimu wake wa kijeshi ndani ya M23 Kanali Bosco Ntaganda – na kumwondoa kama kamanda wa wapiganaji wa M23.

Ntaganda alikimbilia nchini Rwanda ambako alijisalimisha kwa ubalozi wa Marekani.

Sasa yuko katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC, akisubiri kufunguliwa mashitaka ya uhalifu wa kivita.

Ikiwa hatafanikiwa kukubaliana na serikali ya DRC, Makenga huenda na yeye pia akafikishwa ICC.

Ingawa hakuna kibali cha kumkamata, baraza la usalama la Umoja wa Mataifa lilimwekea vikwazo vya usafiri pamoja na kupiga tanji mali zake, mwaka jana likimtuhumu kwa kuongoza uasi wa M23 na kuwafanyia ukatili raia wa Congo, Mashariki mwa nchi.

Lakini kulingana na kanali Makenga, alipigana vita halali akitetea haki za jamii ya watutsi.

Mwaka huu wote kumekuwa na tetesi kua yuko katika hili mbaya ya kiafya na kujisalimisha kwake ni ishara kuwa huenda asirejee tena vitani.


ALIEVUNJA NDOA YA BOB JUNIOR AKANUSHA HABARI HIZO.

 

Baada ya Blogs na Magazeti Kumwandika sana Ashley Toto  Mwanadada Kutoka Kenya Kuhusika na Kuvunjika kwa ndoa ya Bob Junior Amejitokeza na Kuandika haya kwenye Wall yake ya Facebook
"****JAMANI NIMECHOKA NA SKEDOLS ZA UONGO ILA NAAMINI HII NI MITIHANI NA INSHAALLAH YATAISHA***I HAVE NOTHING TO DO WITH HIM...." 

Tuliamua kumtafuta na kuongea nae na kusema kwa masikitiko kuwa Hana uhusiano wa kimapenzi na Bob Junior Bali wao ni marafiki tu wa Muda mrefu..Pia akasema huwa anamtafutia Show Sehemu mbali mbali ikiwemo Ujerumani anapoishi ..... So anasema amechoka kuandikwa kuhusu Bob Junior


JOHN MNYIKA NAE ASEMA YAKE KUHUSU ISHU YA ZITTO KABWE KUPOKEA PESA TOKA C.C.M


Mgogoro ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), umeingia katika sura mpya baada ya viongozi wake wawili waandamizi, Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe na Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo kuuandikia uongozi wa chama hicho wakitaka uikane taarifa inayowachafua mitandaoni.

Zitto na Dk Mkumbo wanatuhumiwa kupokea fedha na kushirikiana na viongozi wa Idara ya Usalama wa Taifa na wale wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa nia ya kuivuruga Chadema.

Taarifa hiy
o yenye kichwa cha habari 'Ripoti ya siri juu ya Zitto Kabwe’, ambayo imesambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii katika siku za karibuni inadaiwa kuwa iliandaliwa na Kitengo cha Upelelezi cha Chadema baada ya uchunguzi wa mwenendo wa Zitto ndani na nje ya nchi kuanzia mwaka 2008.

Sehemu ya taarifa hiyo ya mtandaoni inadai kuwa Zitto alipelekewa kiasi cha Dola za Marekani 266,000 (Sh416 milioni) huko Ujerumani na maofisa wa Usalama wa Tanzania, Desemba 16, 2009.

Ripoti hiyo inadai kuwa fedha hizo zilipitishwa katika Benki ya Berliner ya Ujerumani kwenye akaunti ya raia wa nchi hiyo, Andrea Cordes, ambaye anadaiwa kumpelelekea Zitto.
Taarifa zaidi zinadai kuwa fedha hizo ziligawiwa kwa wafuasi mbalimbali wa chama hicho na miongoni mwao ni Dk Mkumbo.

Zitto amlima barua Dk Slaa
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Zitto alisema amemwandikia barua Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa kumwomba athibitishe ‘Taarifa ya Siri ya Chadema’ kama ni ya kweli au chama hicho kiikanushe ili aweze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa kile alichokiita ‘hekaya.’

“Taarifa ya Chadema inasema kwamba chama hicho (chama changu), kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa mimi ninapokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema,” alisema Zitto kwenye taarifa yake.
Zitto alisema taarifa hiyo ni ya kutunga na iliyojaa uongo wa kiwango cha kutisha, imemfedhehesha, imemsikitisha na kumkasirisha.

Alisema taarifa hiyo iliibuliwa katika kipindi ambacho alikuwa ziarani barani Ulaya katika nchi za Uswisi na Uingereza ambako alikuwa anafuatilia fedha zilizofichwa na Watanzania katika nchi hizo.

“Pengine lengo la ripoti hiyo lilikuwa ni kutaka kunipoteza kutoka katika nia na dhamira yangu ya dhati ya kutaka Watanzania wafaidike na utajiri wao. Muda ambao watunzi wa ripoti hiyo waliamua kutoa taarifa yao unazua maswali mengi kuliko majibu,” alieleza Zitto katika taarifa yake.
Dk Mkumbo alia na uenezi
Dk Mkumbo alieleza kusikitishwa na Idara ya Uenezi ya Chadema kwa kukaa kimya bila kutoa maelezo juu ya suala hilo.

“Hasa pale ambapo tumeambiwa waraka huu umetoka makao makuu. Hii si kawaida kwa idara yetu hii nyeti iliyosheheni watu mahiri. Mara zote huwa wepesi kabisa kwa vijana wetu katika idara hii kutoa ufafanuzi, tena kwa mambo mepesi kabisa yanayokigusa chama, vipi makamanda kwenye jambo hili imekuwaje?” aliandika Dk Mkumbo kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Facebook jana na kuthibitisha kwa simu.

Dk Kitila alis
ema pamoja na umaskini wake, hajawahi kuhongwa popote na wala hatarajii.
“Taarifa zinazosambazwa kuhusu mimi ni za uongo wa kijinga na uzushi wa kitoto kwa malengo ya siasa nyepesi. Ni wazi kwamba wanaosambaza habari chafu kunihusu hawanijui na ndiyo maana wanaweza kudiriki kuzusha kwamba mimi Kitila Mkumbo naweza kuhongwa Sh200,000.”

Alihoji pia Chadema ilikuwa na siri gani za hatari kiasi cha kumfanya Zitto, ambaye ni rafiki yake wa siku nyingi kuhongwa kiasi hicho kikubwa cha fedha.
Mnyika awajibu
Hata hivyo, Katibu Mwenezi wa Chadema, John Mnyika ameikana ripoti hiyo na kueleza kuwa haijaandikwa na makao makuu ya Chadema.

Mnyika alisema Zitto ameibua kitu ambacho anafahamu kuwa kimeshughulikiwa na uongozi wa chama hicho.
“Zitto anajua kuwa Andrea Cordes aliniandikia baruapepe na nakala kwake nikawajibu kuwa ripoti hiyo haijaandikwa na Makao Makuu ya chama na tukipokea malalamiko rasmi tutachunguza kwa sasa chama kinaichukulia ripoti hiyo kama ripoti nyingine zinazosambazwa mitandaoni,” alifafanua Mnyika.

Akizungumzia malalamiko ya Dk Mkumbo, Mnyika alisema alikuwa anapaswa kufuata taratibu za chama kama alikuwa na malalamiko.

Alisema baada ya taarifa hiyo ya siri kusambaa mtandaoni, Zitto alitoa kauli na kama Dk Mkumbo hakuridhika, alipaswa kuonana na watu wa Idara ya Uenezi ya Chadema.
“Idara ingetoa ufafanuzi zaidi. Mjadala huu usikuzwe bila sababu za msingi na kufunika masuala mengine muhimu ya kitaifa,” alisema Mnyika.
Chanzo: Mwananchi