Monday, December 30, 2013

MAISHA NI MAPAMBANO,HAPANA KUCHOKA.

Kila mwananchi wa nchini au taifa lolote Duniani anahitaji kuishi katika mazingira mazuri ambayo yatamfanya awe na furaha na amani muda wote kutokana na mazingira anayoishi kwanza.Lakini kutokana na mambo mbali mbali ambayo aidha watu wamejisahau au jamii inayowazunguka kushindwa kuwakumbusha kwa kufanya mambo kadhaa nao wameshindwa kukumbuka wapi walipo.
Hii ni nyumba ambayo mtu anaishi na anaendeshea maisha yake hapa kwa muda mrefu sana.Sasa swala laja kuwa huyu mkazi anaekaaa katika mazingira haya anaweza kumsisitiza mtoto wake aweze kwenda shule ili aweze kumkomboa mzazi wake kutoka katika mazingira haya?.Pia ni wazazi wachache sana ambao wanauwezo huo kutokana na wengine huishi katika hali ngumu sana za kimaisha kiasi kwamba wengine wanauwezo wa kupata mlo wa mmoja kwa siku au siku zingine hamna kabisa.
Maisha ya sasa ni ya kupambana na sio ya kubweteka na kukaa vijiweni kutokana kwamba vijiwe hivyo hivyo huleta maandeleo na pia kupitia vijiwe hivyo hivyo pia huwapeleka vijana wengi katika mstari tofauti na ule ambao walikuepo awali.
Naamini kwa kupitia changamoto unazokutana nazo unaweza kufanya kitu ambacho kitakua tofauti na kupitia wewe unaweza kusababisha watu wengine wakatoka sehemu waliyokuwapo na kwenda sehemu nyingine.HAKUNA KINACHOSHINDIKANA CHINI YA JUA KAMA UNAJITAMBUA ANZA SASA.


No comments:

Post a Comment